Didmus Barasa Atamatisha Likizo, Ampigia Debe Mgombea wa UDA Kiambaa

August 2024 ยท 2 minute read

Mbunge wa Kimilili Didmus Barasa amerejea katika ulingo wa siasa baada ya kuchukua mapumziko ya miezi mitatu.

Habari Nyingine: Juja: Dereva Afariki Dunia Baada ya Genge Kumiminia Gari Lake Risasi

Barasa Jumanne, Juni 22, alionyesha dalili wazi kwamba huenda asitengane na kambi ya Naibu Rais William Ruto baada ya kumpigia debe mgombea wa United Democratic Alliance Njuguna wa Wanjiku eneo la Kiambaa.

Mbunge huyo aliyechaguliwa kwa tikiti ya Jubilee katika Uchaguzi Mkuu wa 2017, alijiunga na mwenzake wa Gatundu Kusini Moses Kuria kwenye harakati za kampeni katika eneo bunge linalodhaniwa kuwa ngome ya Rais Uhuru Kenyatta.

Habari Nyingine: Magazeti ya Jumatano, Juni 23: Uhuru Kupiga Ziara Katika Ngome ya Ruto Bonde la Ufa

Mbunge huyo mchanga katika video iliyoonekana na TUKO.co.ke, alidokeza atamuunga mkono Ruto kwa urais wa 2022.

"Rafiki zako ni akina nani? Mbele ni DP Ruto, akifuatiwa na Moses Kuria na Didmus Barasa yupo akiwapongeza," Barasa alisema.

Mwanasiasa huyo alizua gumzo Jumapili, Machi 21, baada ya kutangaza atachukua likizo ya miezi minne kutoka kwa siasa za kitaifa.

Habari Nyingine: Gavana Kibwana Asema Alishuhudia Raila Akiahidi Kuunga Kalonzo Mkono 2022

Alisema kwamba atatumia mapumziko kushauriana juu ya hatua yake ya kisiasa ijayo na wafuasi wake na pia kuzingatia mambo ya Mulembe taifa.

"Tunapotii mwito wa Rais Uhuru Kenyatta wa kupunguza shughuli zetu za kisiasa kudhibiti kuenea kwa COVID-19, nitachukua wakati huu kuchukua likizo ya sabato kwa karibu miezi minne kusaidia taifa la Mulembe," alisema.

Mbunge wa Tanga Tanga baadaye Jumatano, Mei 12, alipunguza likizo yake hadi miezi miwili.

Barasa alisema aliamua kupunguza kipindi hicho hadi miezi miwili baada ya kufanikiwa kuwashirikisha wafuasi wake na uongozi wa kisiasa wa Mulembe kupata mwelekeo wake.

''Katika miezi miwili iliyopita, nimekuwa likizoni, niliwasiliana na viongozi kadhaa wa Mulembe. Bado ningali ninaendelea na mzungumzo na wengine wao," alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZoN1gpFmm6KcnarAbq7Aq5ismV2WwaK5wK2grKCRYrmqt8izpmaZnaW2qLXAZpuempViuqi7zJucmmWnlnq2sMBmoqKZnZeuonrHraSl